Pages

Sample Text

Frank Kimaro run this blog

11/13/2012

Wafanyakazi TAZARA wagoma


Na Frank Kimaro
Wafanyakazi wa Tanzania and Zambia Railway (TAZARA) waliopo kanda maalumu ya Dar es salaam jana walifikia maamuzi ya kutokufanya kazi mpaka mkurugenzi wa shirika hilo atakapokubali kuzungumza nao.

Wafanyakazi hao walitoa rai hiyo baada ya mkurugenzi wa shirika hilo kukataa kuzungumza nao akitoa sababu kwamba hakuwa tayari mpaka Jumatatu ya wiki ijayo ndipo ataweza kuzungumza juu ya matakwa yao.

Baadhi ya abiria wakisubiria treni wakati mgomo wa wafanyakazi ukiendelea. 

Wafanyakazi hao waliweka bayana madai mbalimbali ambayo shirika hilo linapaswa kuwatimizia lakini bado mpaka sasa hayajatimizwa na hakuna sababu za msingi zilizotolewa na kiongozi uongozi mkuu wa shirika hilo katika kushindwa kutimiza matakwa yao.

“Hatujapata mishahara ya miezi miwili yani wa 9 na wa 10 na sasa tunaelekea katikati ya mwenzi wa 11, hatuelewi hatima yetu wakati sisi pia tuna majukumu kama binadamu wengine”Alisikika akisema mmoja wa wafanyakazi ambaye hakupenda jina lake litajwe.

Mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi wa reli (TRAWU) kanda maalumu ya Dar es salaam Bw Yusufu Mandai alisema madai yanayotolewa na wafanyakazi  wenzake ni ya msingi na yanapaswa kutiliwa maanani kwa sababu mshahara ni haki yao ukizingatia wanafanya kazi.

“Watu wanaishi kutokana na mishahara inayopatikana hapa si vyema watu kufanya kazi mienzi miwili mfululizo bila kulipwa mishahara yao,” alisikika akisema.

Msemaji mkuu wa TAZARA, Bw Conrad Simuchile ameliambia gazeti hili kwamba kwa sasa shirika hilo haliko tayari kuzungumzia juu ya hali hiyo lakini itatoa tamko siku za karibuni.

“Shirika litatoa kauli kuhusiana na hali inayoendelea katika siku chache zinazokuja,” alisema Bw Simuchile.

No comments:

Post a Comment

COMMENT HAPA UKIMALIZA, KWENYE PROFILE SELECT ANONYMOUS KISHA BONYEZA PUBLISH.