Pages

Sample Text

Frank Kimaro run this blog

4/19/2012

Yanayoendelea katika chuo kikuu cha Tumaini Iringa kabla ya Uchaguzi mkuu chuoni hapo

                             Vijana wakiwa wanasubiri wagombea wao kuja kuanza kunadi sera zao

      Aliyekuwa naibu waziri wa habarih(Catherine Moshi) akiwa na mwalimu wake(Mr. Damalo) kabla ya    kuanza kuwasikiliza wagombea mbalimbali

   Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi(Edo Mfungo) akiwa anamtambulisha mgombea wa Uraisi Joshua Chussi

    Mshauri wa wanafunzid(Hosward Ndelwa) alisimama kuwakanya wanafunzi pale kelele zilipozidi

                   Mgombea wa kiti cha uraisi Mauna Chuma akiwa anazinadi sera zake

                          Mmoja kati ya wagombea wa kiti cha makamu wa raisi Judith Kahwa

                 Shabiki huyu alshindwa kuhimili hisia zake na kujikuta amepanda juu ya dawati akishabikia

4/17/2012

Mwanafunzi wa Tumaini Iringa ungependa kuwa na raisi wa aina gani?

Kuanzia kulia ni mgombea wa uraisi Mauna Chuma akiwa na Mpoki Ndimyaki (kati) ambaye ndiye mratibu wa kampeni za mgombea huyo pamoja na Humphrey Kusika

MAONI YA WADAU KUHUSU RAISI WANAYEMTAKA

                                  Awe anajali masela walio gheto wanaoteseka

                                        Mimi kwanza kura sipigi maana sikubali kudanganyika

                              Kwanza uongozi uliopita ungetuambia elfu kumi na nane zetu umepeleka wapi

                                          Inabidi aruhusu hata bodaboda zipaki ndani ya chuo

Raisi akiwa sharobaro itakuwa poa sio habari za kichungaji

Raisi awe mtu wa watu mara mojamoja awe anatokea hata kwenye birthday

                                       Anatakiwa awe muwazi sio fisadi kama baadhi ya waliopita

                                             Awe anajali hata michezo kidogo

                                  Akiwa mnywaji kama yule mwingine pia sio mbaya ila asiwe fisadi

4/15/2012

Tumaini University yaichabanga Ruaha University 38-34 katika mchezo wa kikapu

                             Faraja Naiman(big) wa Tumaini akiwa anaenda kudaka mpira kabla mechi haijaanza

                   Maxwell mchezaji wa Tumaini akiwa anapenya vizuri kabisa kwa ajili ya kwenda kufunga

           Kocha wa timu ya Tumaini Renatus Mgongo akiwa an anatoa maelekezo kwa wachezaji wake

                               mchezaji wa Tumaini baada ya kuanguka katika mchezo huo

                            shabiki maarufu kama Masai akiwa anashabikia mchezo huo

                Mchezo ulivyozidi kuwa mgumu RUCO wakaitana kidogo waelekezane baadhi ya mambo